1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAsia

Watu 48 wafariki baada ya barabara kuporomoka China

2 Mei 2024

Idadi ya watu waliofariki kufuatia mmomonyoko wa udongo kwenye barabara kuu katika mkoa wa Guangdong kusini mwa China imeongezeka hadi watu 48 huku wengine 30 wakijeruhiwa.

https://p.dw.com/p/4fQH6
China Guangdong Meizhou | Barabara ilioharibika kufuatia mmomonyoko wa udongo.
Wafanyakazi wa uokoaji wakiendelea na uokozi eneo lilioathirika na mmomonyoko wa udongo China.Picha: VCG/IMAGO

Hayo ikiwa ni kulingana na vyombo vya habari vya serikali ambavyo vimeeleza pia kuwa juhudi za uokoaji zinaendelea.

Hapo jana, sehemu ya barabara inayotoka katika jiji la Meizhou kuelekea kaunti ya Dabu iliporomoka kutokana na mvua kubwa zilizonyesha eneo hilo, jambo lililopelekea magari kadhaa kuanguka kwenye korongo la karibu mita 18. 

Soma pia:Iran na China zatia saini makubaliano ya ushirikiano

Katika wiki za hivi karibuni, mji wa viwanda na wenye watu wengi wa Guangdong, umekuwa ukikumbwa na msururu wa majanga yatokanayo na hali mbaya ya hewa ikiwa ni pamoja na dhoruba.

China hutoa idadi kubwa ya gesi chafuzi kwa mazingira lakini imeahidi kupunguza maradufu uzalishaji huo ifikapo mwaka 2060.